Na Esther Mnyika, Dar es Salaam
JUMLA ya Wanafunzi 1,172,279 wa darasa la saba waliopo katika shule za msingi Tanzania Bara jumla ya shule 19,441 wanatarajia kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kuanza kesho Septemba,10 hadi 11 2025.

Amesema kati yao wavulana ni 535,138 sawa na asilimia 45.65 na wasichana ni 637,141 sawa na asilimia 54.35.
Akizungumza leo Septemba, 9 2025 Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), Profesa Said Mohamed amesema kati ya watahiniwa 1,172,279 waliosajiliwa kufanya mtihani mwaka 2025.
” Watahiniwa 10, 94,321 sawa na asilimia 93.35 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili na watahiniwa 77, 958 sawa na asilimia 6.65 watafanya mtihani kwa lugha ya kingereza ambayo wamekuwa wakitumia katika kujifunzia,”amesema Profesa Mohamed.
Ameongeza kuwa watahiniwa wenye mahitaji maalumu waliosajiliwa kufanya mtihani huo ni 4,679 kati yao ni 92 wasioona,1,551 wenye uono hafifu, 1,079 wenye uziwi, 448 ni wenye ulemavu wa akili na1,509 wenye ulemavu wa viungo.
Profesa Mohamed ameeleza kuwa katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi nijumla ya masomo sita ambayo ni Kiswahili, English Language, Sayansi na Teknolojia/Science, Hisabati, Maarifa ya Jamii na Stadi za Kazi pamoja na uraia.
Pia amezitaka shule na wanafunzi wote kuepuka vitendo vya udanganyifu, likisisitiza kuwa halitasita kufuta matokeo ya yeyote atakayebainika kushiriki katika vitendo hivyo.



