Home SIASA DK. Mwinyi: Serikali itahakikisha hospitali zote zinatoa huduma za kibingwa

DK. Mwinyi: Serikali itahakikisha hospitali zote zinatoa huduma za kibingwa

Na Esther Mnyika, Zanzibar 

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema  Serikali itahakikisha hospitali zote zinatoa huduma za kibingwa ikiwemo Hospitali ya Abdallah  Mzee kupatiwa mashine ya MRI.

Akizungumza Septemba,24 2025 Dk. Mwinyi  kwenye mkutano wa kampeni  uliofanyika Makombeni,Wilaya ya Mkoani  Mkoa wa Kusini Pemba  amesema kasi ya maendeleo yaliyopatikana  katika  kipindi vha miaka mitano iliyopita itongezeka zaidi kupitia miradi mikubwa ya maendeleo.

“Serikali italeta mashine ya MRI   hapa hapa pemba mashine ya kusafisha damu ma figo kuletwa pemba hakuna watu kusafiri kwenda Dar es Salaam  au nje ya nchi kupata huduma  hapa hapa  na  kuhakikisha mnapata huduma bora,” amesema.

Akizungumzia kuhusu zao la karafuu Dk. Mwinyi amesema  serikali itaendelea kulipa kipaumbele zao hilo ikiwa ni zao kuu la uchumi na kuliongezea thamani. 

“Bei ya karafuu haijabadilika na haitabadilika asilimia 20 inachukua serikali kwaajili ya huduma  na asilimia 80 anachukua mkulima  hivyo zao la karafuu tutaendelea  kulienzi  na linahitajika duniani,”amesema.

Ameongeza kuwa akipewa ridhaa ya kuwa rais kipaumbele cha kwanza itakuwa ajira kwa vijana serikali kuhakikisha vijana  wengi wanapata ajira serikali, sekta binafsi na kujiajiri. 

Dk. Mwinyi amesema uchumi wa bluu ni sekta mama hivyo kutoa mikopo  kwa wakulima wa mwani na wavuvi na boti kwaajili ya shughuli zao mbalimbali. 

“Hivi karibuni serikali inatarajia kuleta boti mbili za kisasa kwaajili ya Unguja,  pemba na Tanga na meli ya Mv mapinduzi 2 tayari kuzinduliwa hivi karibuni, ” amesema. 

Dk.Mwinyi  amewataka Wanzabar kuepuka siasa za kikanda, kidini, ubaguzi na mifarakano amani na mshikamano ni nguzo kuu za maendeleo 

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kudumisha amani, maridhiano na mshikamano ili kutekeleza mipango ya maendeleo yenye manufaa kwa wananchi wate.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here