Home KITAIFA Mashimo: Viongozi wa dini kusimamia pamoja ili kuleta amani ya nchi

Mashimo: Viongozi wa dini kusimamia pamoja ili kuleta amani ya nchi

Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

MCHUNGAJI wa Kanisa Christian Assembly, Daudi Mashimo ametoa wito maalum kwa viongozi wa dini wa madhehebu yote kusimama pamoja  ili kuleta  amani ya  nchini.

Pia amesema Viongozi wa dini  Waislamu na wakristo wawe pamoja katika  kurudishi  Taifa kuwa pamoja na kuwa wavumilivu kipindi hiki wakati  Tume  ya Uchunguzi Oktoba, 29 2025 inafanya kazi.

Akizungumza  leo Disemba,  23 2025 Jijini Dar es salaam Mchungaji  Mashimo mapema leo wakati a ametoa pole na faraja kwa ndugu na jamaa wote waliopoteza wapendwa wao, akisisitiza kuwa Taifa limepitia mapito mengi yanayohitaji mshikamano na subira.

“Kipindi hiki tuwa wavumilivu huku makanisa  na madhehebu yote tulinde amani  hakuna  serikali  iliyo kamilika duniani  naomba tuwe na subra na hakuna  asiyejua kilichotekea Oktoba,  29 2025  tuwe na subira  wakati Tume inafanya  kazi  kwa kilichotokea,”amesema  Mashimo.

Amesema Katika  kipindi hiki cha kuelekea sikukuu ya Christmas viongozi wa dini kutoka  madhehebu yote wanapaswa kuwa kitu kimoja ili kuhakikisha Taifa linapata faraja, amani na utulivu, badala ya kutumia maumivu ya wananchi kama nyenzo ya kuchochea migawanyiko

“Tunapokwenda kusherekea sikukuu, naomba viongozi wa dini tuwe pamoja, siyo kipindi cha Watanzania kutupiwa mizigo ya kuwaumiza,” amesema.Viongozi  wadini kusimamia kwa pamoja kuleta  amani  nchini 

Mchungaji Mashimo amesema  hakuna Serikali yoyote duniani iliyokamilika, hivyo mshikamano wa kitaifa ni muhimu wakati wote.

Amesema kuwa Sikukuu ya Krismasi inapaswa kuwa chombo cha kuwaunganisha Watanzania ili wawe kitu kimoja na kujenga Taifa lenye upendo na uvumilivu.

“Nipo upande wa Mungu ambaye yupo katika dhamana ya nchi hii, akiongeza kuwa maumivu yaliyopo yasigeuzwe fimbo ya kukumbushana matatizo, bali yawe msingi wa kujenga na kuimarisha Taifa,”amesema.

Aidha amewatakia  Watanzania Krismasi njema, akisema ni maombi yake Yesu Kristo azaliwe upya katika mioyo ya watu wote.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here